Wazee wa Agikuyu na Kalenjin wazungumzia amani

Wazee wa jamii za Agikuyu na wakalenjin katika kaunti ya Uasin Gishu wameanza kuandaa mikutano ya amani ili kuzileta pamoja jamii zote zinazoishi kaunti hiyo.
Wakiongozwa na Joseph Wainaina na Meja mstaafu John Seii, wamesema kwamba walichukua hatua hiyo ili kumaliza wasiwasi uliozuka katika kaunti hiyo baada ya baadhi ya waathiriwa wa machafuko ya kisiasa ya mwaka 2007/08 kutoka kaunti hiyo kuhudhuria mkutano na mkurugenzi wa DCI mwezi uliopita kurekodi taarifa.
Wakizungumza kule Eldoret kadhalika wamewataka wanasiasa kutotumia siasa kuwagawanya wananchi eneo hilo wakisema kamwe hawatamuunga mkono mwanasiasa yeyote ambaye atakua na nia kama hiyo.